15 Agosti 2025 - 10:25
Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber, Arejea Nchini Baada ya Kikao cha Kimataifa Nchini Misri

"Tumejadili namna bora ya kumaliza mzozo huo kwa njia ya amani. Na tunawaombea ndugu zetu wa Gaza ili Mwenyezi Mungu awape amani na kumaliza mgogoro huu wa muda mrefu,"

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mheshimiwa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber bin Ally, amerejea nchini akitokea Jamhuri ya Kiarabu ya Misri alikohudhuria kikao cha kimataifa cha Mamufti kilichofanyika kwa muda wa siku mbili.

Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber, Arejea Nchini Baada ya Kikao cha Kimataifa Nchini Misri

Akizungumza baada ya kurejea, Mufti amesema kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali yanayohusu changamoto na fursa za dunia ya sasa, ikiwemo matumizi ya teknolojia ya akili bandia (AI). 

"Hatuwezi kuiepuka, kwani dunia imefika hapo kwa sasa. Hata hivyo, tusiipe nafasi kubwa katika kutatua matatizo ya masuala ya dini na elimu, kwani mwanzilishi wake ni mwanadamu. Zipo taarifa tunazoweza kuzitafuta kupitia AI, lakini sio kutegemea kila kitu kutoka kwake," alisema Mufti.

Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber, Arejea Nchini Baada ya Kikao cha Kimataifa Nchini Misri

Aidha, Mufti alieleza kuwa kikao hicho pia kilijadili hali ya Wapalestina na njia zinazoweza kufanikisha amani ya kudumu katika eneo hilo.

"Tumejadili namna bora ya kumaliza mzozo huo kwa njia ya amani. Na tunawaombea ndugu zetu wa Gaza ili Mwenyezi Mungu awape amani na kumaliza mgogoro huu wa muda mrefu," aliongeza Mufti.

Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber, Arejea Nchini Baada ya Kikao cha Kimataifa Nchini Misri

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha